Sunday, July 14, 2013

UTAGUNDUAJE KAMA UNA MIMBA CHANGA?


Mara nyingi ni vigumu mwanamke kugundua kama ameshika mimba siku za mwanzoni hadi pale anapokosa kuona siku zake za hedhi. pamoja na ugumu huo kuna dalili ambazo zinaweza kufanya uhisi kama una mimba katika siku za mwanzoni ambazo ni kuanzia siku ya 18 toka mimba itungwe.

Dalili hizi zinatofautiana kwa kila mtu, wapo ambao wanaweza kuzipata zote na ambao hupata baadhi tu ya dalili hizi na pia wapo ambao hawazipati kabisa.

Miongoni mwa dalili hizo ni pamoja na:

1.JOTO LA MWILI KUPANDA.(basal body temperature stay high)

Wanawake wengi hushindwa kutambua dalili hii pale wanapoipata kutokana na kutokuwa na uelewa
juu ya miili yao.
Hali hii inaonekana katika siku za mwanzo ambambo huweza kudumu kwa muda mrefu kiasi hivyo
kama itadumu zaidi ya siku 18 basi ni vizuri kupima ili kujua kama inatokana na ujauzito au la.

2. KUPATA HAJA NDOGO MARA KWA MARA.(frequent urination)
Kubanwa na haja ndogo mara kwa mara pia inaweza ikawa ni dalili mojawapo ya kuwa na mimba
changa.

3.KUWA MWEPESI KUHISI HARAFU YA VITU MBALI MBALI HASA HARUFU MBAYA.(sensitivity to odors)
Wakati wa mimba changa wanawake wengi wanakuwa wepesi wa kuhisi harufu ya vitu mbali mbali hasa zile harufu zisizo za kupendeza na kumfanya achukie vitu vingi vyenye kutoa harufu hizo.
wakati kama huu si ajabu ukaona mtu hataki mume wake amsogelee kwa kudai anatoa harufu mbaya.
ukiona dalili kama hii inaweza ikawa ni ishara ya kuwa mjamzito hivyo unapaswa kufanya uchunguzi.

4.KUKOSA HEDHI.(missed period)
Kwa kawaida mama mjamzito hapati siku zake za hedhi isipokua anaweza akapatwa na hali ya kuvuja kunakofanana na ile ya hedhi ila damu yake huwa nyepesi sana na hudumu kwa muda mfupi kati ya siku1 au 2 (implantation bleeding) hivyo unapokosa kuona siku zako za hedhi
unapaswa kuchunguza sababu za kukosekana kwa hedhi.

5. KICHEFU CHEFU AU KUTAPIKA.

No comments:

Post a Comment